Yesu Unipendaye by 1 composer

Lyrics

Follow the words comfortably while rehearsal tools stay close by in the sidebar.

0 audios Video guide

Verse 1

Yesu unipendaye, kwako nakimbilia,

Ni wewe utoshaye, mwovu akinijia.

Yafiche ubavuni, mwako maisha yangu,

Nifishe bandarini, wokoe moyo wangu.

Verse 2

Ngome nyingine sina, nategemea kwako,

Usinitupe Bwana, nipe neema yako,

Ninakuamania, mwenye kuniwezesha,

Shari wanikingia, vitani wanitosha.

Verse 3

Nakutaka Mpaji, vyote napata kwako,

Niwapo mhitaji, utanijazi vyako,

Nao waangukao, wanyonge wape nguvu,

Poza wauguao, uongoze vipofu.

Verse 4

Bwana umeniosha, moyo kwa damu yako,

Neema ya kutosha, yapatikana kwako,

Kwako Bwana naona, kisima cha uzima,

Mwangu moyoni Bwana, bubujika daima.

Comments 0 110 views

Log in to add a comment

No comments yet. Be the first to comment!

More by Anonymous

From the Blog